Aunt Ezekiel Atumbuliwa Jipu Na Serikali Ya Magufuli, Ipo Hapa



Kaulimbiu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli ‘JPM’ ya kutumbua majipu na watu wasiolipa kodi imemdondokea staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson baada ya gari lake aina ya Audi kukamatwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa tuhuma za kuingizwa nchini kinyemela bila kulipiwa ushuru na kukwepa kodi.

Habari kutoka kwa vyanzo vya kuaminika zilieleza kuwa tukio la Aunt kutumbuliwa lilijiri hivi karibuni ambapo staa huyo alikuwa akificha siri hiyo isinaswe na mapaparazi wetu, jambo ambalo limemshinda.



Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, Wikienda lilimsaka Aunt kutaka kujua kisa kamili ambapo alipobanwa alikiri kukamatwa kwa gari lake hilo kwa makosa ya kukwepa kodi wakati linaingizwa Bongo hivyo kuwa mikononi mwa TRA.

“Kweli gari langu limeshikiliwa na TRA ila haina tatizo sana kwani wamekagua, karibia kila kitu kipo sawa isipokuwa ninadaiwa kodi tu ambayo nayo si fedha nyingi kiasi cha kunishinda. Waliniambia vibali vyake vyote viko sawa na kwamba lipo nchini kihalali kabisa hivyo ninachotakiwa kulipia ni kodi tu ambayo najipanga kulipia muda wowote.

“Nilishtuka sana baada ya kukamatwa kwani nilihisi ndiyo mwisho wa kuwa na gari langu lakini sasa nimepata moyo baada ya kuambiwa hakuna kilichochakachuliwa.


“Natafuta Sh. milioni 10 na kitu ili niweze kulikomboa,” alisema Aunt aliyedai gari hilo alinunuliwa na baba mtoto wake, Moses Iyobo ‘Moze’ huku akigoma kutaja bei yake.

-GPL

Haya Ndio Maisha ya Mbunge SUGU Kwa Dasa


Kwenye Kampeni za uchaguzi Mkuu wa 2010 na 2015, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu alijishusha na kujinyongesha ili wananchi wamwamini na kumpa kura. Miongoni mwa mambo aliyotumia kuombea kura ni kutomiliki Magari na Nyumba za Kifahari na badala yake atatumia fedha atakazopata kuwahudumia wananchi hasa kwenye huduma za Afya na Elimu. Moja ya ahadi kuu ya Mr Sugu ni hii hapa na nanukuu;

========="Nikichaguliwa kuwa Mbunge, sioni faida ya kutembelea magari ya kifahari na kulala kwenye jumba la kifahari wakati wananchi wangu wanateseka kwa kukosa huduma bora hospitalini na watoto wanakosa vitabu, vyumba vya madarasa na madawati. Nitauza mpaka gari la Mkuu wa Mkoa ili kuhudumia Jamii========= Mwisho wa Kunukuu.

Sasa linganisha kauli hiyo na haya maisha anayoishi Mbunge wa Mbeya Mjini, Mr Sugu. Je kwa tafsiri yako msomaji, nini maana ya Magari ya Kifahari na Nyumba ya kifahari? Hivi anavyomiliki Sugu si vitu vya kifahari?

Jack Wolper Adaiwa Kutolewa vyombo nje na Mwenye Nyumba......

STAA wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper ambaye hivi karibuni ameonekana kulegalega amedaiwa kutolewa vyombo vyake nje kwenye nyumba aliyokuwa amepanga maeneo ya Mikocheni jiji Dar.
Chanzo chetu makini kabisa kinadaiwa kuwa kipindi staa huyo akiwa nchini Afrika Kusini aliwaacha ndugu zake kwenye nyumba hiyo lakini kwa kushindwa kulipia kodi kwa kipindi kinachotakiwa, kabla hata hajarejea mwenye nyumba aliamua kutoa vitu nje na ndugu wa staa huyo kila mmoja kuelekea anakokujua.

“Maskini, wakati Wolper yupo Afrika Kusini aliwaacha ndugu zake kwenye nyumba hiyo lakini ilishindikana kulipa kodi hivyo mwenye nyumba aliwatimua ndugu zake,” kilisema chanzo hicho.
Kilizidi kufunguka kuwa, baada ya Wolper kurejea nchini ilibidi kuishi hotelini mpaka sasa ili kukusanya fedha nyingine kwa ajili ya kupanga nyumba ambayo ataweza kuishi pamoja na ndugu zake.

“Wolper na mpenzi wake tangu waliporejea nchini wanaishi hotelini, nafikiri wanajipanga ili waweze kupata fedha za kuweza kupanga tena nyumba kama ilivyokuwa huko nyuma,” kilisema chanzo hicho.

Gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Wolper kwenye simu ambapo alipoulizwa kama ni kweli ametolewa vitu nje, alijibu;

“Hao wanaosema nimefulia hadi kutolewa vitu nje ni wazushi tu, hawana nia njema na mimi, najua ninachokifanya mjini hivyo hawanipi shida, wache waseme mpaka wachoke.”

MPYA Kuhusu Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi (Dart)...Tarehe ya Kuanza Kazi Yatajwa Rasmi...

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene amesema mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi (Dart), unatarajia kuanza rasmi Mei 10, mwaka huu.

Akizungumza kwenye majumuisho ya ziara ya Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Simbachawene alisema baada ya kukutana na wadau wa mradi huo, wamewahakikishia kuwa utaanza rasmi mwezi ujao bila kukosa.

“Tumeambiwa mradi huu una mikataba mingi na kuwa bado kuna mjadala mkubwa wa mikataba. Hatuwezi kulazimisha maana unaweza kujikuta ukitengeneza mikataba mibaya, hivyo tunaendelea na mijadala ya mikataba,” alisema.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jasson Rweikiza alisema wameutembelea mradi huo zaidi ya mara nne na kugundua tatizo linaloukwamisha kuwa ni fedha na kuitaka Serikali kutoa fedha ili uanze.

Aliesema lengo la kuanzishwa kwa mradi huo ni kupunguza kero ya usafiri kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wanaokabiliwa na tatizo la usafiri na foleni za barabarani, hivyo kutumia muda mrefu barabarani.

Rweikiza alisema kukamilika kwa mradi huo na kuanza kufanya kazi kutapunguza kero na kuokoa muda mwingi uliokuwa ukitumia bila uzalishaji.

Tuhuma za Mwanamuziki TID Kutumia Madawa ya Kulevya...Mwenyewe Afunguka

Baada ya KR kujitambulisha kuwa yeye ndiye Rais wa RADA Entertainment na Juma Nature kumpinga kwa kejeli akisema hamtambui Rais yoyote zaidi ya Rais Magufuli hatimaye TID anyoosha maelezo.


T.I.D amesema muda ukifika watamuapisha rasmi KR Mulla kuwa Rais wa Radar Entertainment na kutoa sababu za kufanya kazi na KR Mulla katika label yake.

Zaidi eNews ilipotaka kupata maelezo ya kina juu ya tuhuma za TID kuhusishwa na matumizi ya madawa ya kulevya, TID aligoma kusema chochote, na hata alipoulizwa juu ya tuhuma hizo kwa wasanii wengine pia TID alisema “Muda ukifika nitaongea nyie endeleeni kuongea vitu msivyovijua”.

Manispaa ya Kinondoni Chini ya CHADEMA Yatangaza Neema Kwa Wakazi Wake..Sasa Kila Mkazi Kupata Bima ya Afya

Manispaa  ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, inayoongozwa na Chama cha Demkrasia na Maendeleo (Chadema), chini ya Ukawa imeanza kazi kwa staili ya aina yake baada ya kutangaza neema ya bima ya afya kwa wananchi wa Manispaa hiyo.

Imeahidi kuanzisha mpango maalum ambao kila mwananchi wa Manispaa hiyo atachangia Sh. 40,000 kwa mwaka ili aunganishwe na mpango wa matibabu wa bima ya afya ambao utawawezesha kupata matibabu ya bure katika hospitali mbalimbali.

Mpango huo utaanza kutekelezwa mwezi Juni mwaka huu, huku bajeti ya Manispaa hiyo ikiongezeka kwa asilimia 59 kutokana na kukua kwa mapato ya ndani.

Wazee wa Manispaa hiyo nao wametangaziwa neema ya matibabu bure kwani watapewa kadi maalum zitakazowawezesha kutibiwa hospitali za umma.

Mapato hayo yametokana na ukusanyaji madhubuti katika kodi za majengo, mabango, leseni za biashara, huduma za kuegesha magari, hoteli na ruzuku ya serikali kuu.

Bajeti ya mwaka 2016/2017 katika Manispaa hiyo inafikia Sh. Bilioni 248.47 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka jana ambayo ilikuwa ya Sh. Bilioni 156.24.

Katika bajeti ya mwaka huu kuna ongezeko la Sh. zaidi ya bilioni 92.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob aliwasilisha bajeti hiyo jana jijini Dar es Salaam katika kikao cha Baraza la Madiwani.

Baada ya kuwasilisha bajeti hiyo, Madiwani wote wakiwamo wa upinzani na Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliipitisha kwa kauli moja ili ianze kuwahudumia wananchi.

Akisoma bajeti hiyo, Jacob alitaja ukusanyaji wa mapato ya ndani umeingiza Sh. bilioni 64.28 na kwamba imeongezeka kutoka Sh. bilioni 56.6 za mwaka jana.

Licha ya bajeti ya mwaka huu kulenga kugharamia huduma za matibabu, lakini imelenga kujenga shule ya bweni katika Kata ya Goba kwa gharama ya Sh. milioni 250, ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule, kujenga vyumba vya madarasa na ununuzi wa madawati 30,000.

Kazi nyingine zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa Barabara kuelekea kituo cha daladala cha ya Simu 2000 na Barabara ya Akachube ambazo zimetengewa Sh. bilioni 50.

Kuhusu suala la usafi, Meya Jacob alisema kila Kata itakuwa na gari lake la kuzolea takataka na Manipaa imetenga Sh. 2.2b .

Manispaa hiyo ina jumla ya Kata 25 na Sh. bilioni 3.6 zimetengwa kwa ajili ya gharama za kusafirisha takataka.

Aidha, katika bajeti hiyo, Manispaa inatarajia kununua Trekta lenye kijiko kwa ajili ya kutengeneza barabara na zimetengwa Sh. bilioni 1 kwa ajili ya kazi hiyo.

Kazi nyingine za fedha hizo ni kuweka sakafu ngumu katika masoko yote ya manispaa, ili kuondoa adha ya uchafu na matope katika msimu wa mvua na zimetengwa Sh. bilioni 1.65.

Kuhusu vijana na wanawake Manispaa hiyo imetenga Sh. bilioni 4.7 kwa ajili ya kuwakopesha na kila Kata itapata Sh. milioni 200.

LEMUTUZ Afunguka Kuhusu Kijana Aliyekamatwa Arusha Kwa Kumwita Rais Bwege..Ailaumu Serikali na Polisi

 Blogger Lemutuz naye amefunguka kuhusu kijana aliyekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kutumia Mtandao wa Facebook kumwita Rais Magufuli Bwege  na kwamba hawezi kufananishwa na Nyerere..

Lemutuz Kayasema Haya..... 
lemutuz_nation Mr. Isaack Jana Arusha akirudishwa Rumande baada ya kushitakiwa na Serikali kwa kumtukana Rais Magufuli kwenye mitandao ya kijamii ....hapa ndipo ninapoilaumu Polisi na Serikali I mean huyu mtu kamtukana Rais juzi tu Jana tayari Mahakamani kwa nini iwe hivyo na kwa wananchi wa Kawaida? ....Sheria ipo now kama kuna njia rahisi ya kuwakamata hawa Cyber Abusers ni kwa nini wanapotukanwa Wananchi wa Kawaida inakuwa almost kama hamna Sheria wala uwezekano wa kuwakamata lakini akitukanwa Rais Mara moja wanapatikana? ....ndio maana ninasema na sisi Wananchi tusimameni tuhesabiwe tukatae hawa watu kutuvurugia amani kwenye Social Media .....tupambane nao hata kama itachukua muda mrefu lakini wapate ujumbe kwamba sio Wananchi wote tupo tayari kuwapa hiyo nafasi tutawatafuta na watafikishwa kwenye Sheria tu hata kama ni Miezi SITA au Mwaka wa kuwatafuta! - le Mutuz 34min

Mwigulu Ahojiwa Masaa Matatu na TAKUKURU..Kisa Hichi Hapa

Wanajamvi, kale kamchezo ka Mwigulu kujiona yupo juu ya sheria na kutoa rushwa kila kona ya Iramba imemtokea puani baada ya kukamatwa na kuhojiwa na Takukuru kwa muda wa zaidi ya masaa matatu.

Wagombea wenzake walijitoa katika kinyang'anyiro tangu tarehe 25 kwa madai ya kufanyiwa rafu hizo na kutoa malalamiko yao huku wakisubiri suala hilo kushughulikiwa ndipo warejee kwenye kampeni.

===========================

Ofisi ya Takukuru mkoani Singida imemuhoji kwa masaa kadhaa naibu waziri wa fedha na aliye kuwa mbunge wa Iramba Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, kwa tuhuma za kukiuka sheria ya garama ya uchaguzi na sheria ya kuzui na kupambana na rushwa.

Akiongea na waandishi wa habari mkuu wa Takukuru mkoani Singida Bwana Joshua Msuya amesema Mheshimiwa Mwigulu Nchemba amekiuka sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11/2007 katika zoezi linalo ndelea la kura za maoni ndini ya vyama vya siasa.

Katika hatua nyingine Bwana Msuya amewatahadharisha wagombea wote wa ngaza mbalimbali watakae jihushisha na kutoa rushwa iwe ya fedha au vitu,vifaa vya michezo, madawati watakuwa wamekiuka sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11/2007 na sheria ya uchaguzi cap.343 r.e 2002 na pia sheria ya garama za uchaguzi namba 6/2010.

Katika jimbo la Singida kaskazini wa tia nia saba ambao wanagombea ubunge kwa tiketi ya CCM, wametishia kujitoa katika kinyanganyiri hicho kufuatia msimamizi wa uchaguzi kumwachia mgombea mwenzao ambaye ndiye mbunge wa jimbo hilo kuto kufuata masharati ya sheria za uchaguzi jambo ambalo limekuwa kero hadi kutumia vijana wa shule kuonyesha vipeperushi vyake wakati wa mkutano wa kujinadi.

ITV haikuishi hapa ilifanya juhudi za kumwona kaimu katibu wa CCM mkoa wa Singida ambaye ndiye msimamizi mkuu wa mkoa Bwana Aluu Segamba, amekiri kuwepo kwa matatizo hayo na kuchukuwa jukumu la kumbadilisha msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo na kumweka mwingine.

Baadhi ya majimbo ya uchaguzi yenye wabunge ambao wameamua kutia nia ya kugombea tena wamekuwa wakioneka wao ni chanzo kimoja wapo kikubwa cha kuvunja mashariti ya uchaguzi na kuwasababishia wenzao kuwa na malalamiko mengi,hadi kufikia hatua ya kuiomba serekali kupeleka maafisa wa takukuru na polisi kwenye mikutano ya kujinadi kugombea ubunge.

BREAKING: Hapa Ndipo Utaipenda Siasa ya Bongo... Unaambiwa Dr. Slaa, Tundu Lissu na John Mnyika hawamtaki Lowassa...Wasusia Mkutano Jana

The fact that Dr. Wilbord Slaa, John Mnyika and Tundu Lissu did not show up on yesterday Lowassa-Ukawa press conference is very crucial… I mean there must be something going on behind the curtains, let’s just wait and see!

KUMEKUCHA: Siasa ni tamuu! Nasikia Dr Wilbroad Slaa amekataa katakata kukubaliana na maamuzi ya kumleta Lowassa Sijui ni kweli Au?!

Anasema bora akae bila Chama kuliko kukaa chama kimoja na Lowassa. Na inaonesha anaungwa Mkono na Lissu, Mnyika na wengine wengi. Utakuwa mchezo wa kupishana huyu anatoka huyo anaingia! Ngoja tusubirie tuone mwisho wake

Hapa Kuna Picha 5 Za Lowassa Na Mkewe Wakikabidhiwa Rasmi Kadi Za CHADEMA


Mhe. Freeman Mbowe (katikati) kulia kwake ni Regina Lowassa (mke wa Lowassa) na kushoto kwake ni Edward Lowassa baada ya kukabidhiwa kadi cha Chadema.
4
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi,  James Mbatia akimpongeza Edward Lowassa punde baada ya kujiunga na CHADEMA chama kimojawapo kinachounda umoja wa UKAWA.
6
Mke wa Edward Lowassa, Regina Lowassa akikabidhiwa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe.
5
Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba akimpongeza Mhe. Edward Lowassa baada ya kujiunga na CHADEMA chama kimojawapo kinachounda umoja wa UKAWA.
3

Sentesnsi 50 Alizosisema Edward Lowassa Leo Wakati Akikabidhiwa Rasmi Kadi ya CHADEMA.......Yapo pia maneno ya Mbowe,Lipumba, Makaidi na Mbatia

1.Nimetumia wiki mbili kutafakari hatma yangu ktk Siasa, najua wengi wamesubiri kwa hamu.

2.Watu wangu wamesema fanya maamuzi magumu.. Namshukuru Mke wangu na familia wamekuwa na mimi ktk kipindi kigumu-

3.Nawashukuru watu wengi waliojitokeza kuniunga mkono wakati natafuta wadhamini-

4.Uchaguzi wa Mgombea CCM ulijaa chuki dhidi yangu, Kamati ya Maadili haikutakiwa kuchagua Mgombea-

5.Kilichotokea Dodoma kinaitwa 'kubaka Demokrasia'

6.CCM iliwatumia vijana wachache kunikashifu na baadae wakapewa Madaraka makubwa

7.Kibaya zaidi kilikuwa kuwanyima Wagombea 38 wa CCM haki ya kujieleza mbele ya Kamati Kuu

8.Nilinyimwa haki ya Msingi ya kusikilizwa na kujieleza CCM, nitakuwa mnafki kusema nina imani na CCM

9.CCM niliyoiona Dodoma sio CCM iliyonilea Kisiasa, mimi km Mtanzania mwenye Uhuru nasema sasa basi

10.Mwalimu NYERERE alisema CCM sio baba yangu wala mama yangu,nimeamua kuanzia leo naondoka CCM na kujiunga CHADEMA

11.Namshukuru sana James MBATIA na Viongozi wa UKAWA kwa kuniamini na kunipokea

 12.Naamini UKAWA tutaondoa mfumo wa Utawala wa Chama kimoja, naomba Watz wajiunge nasi ktk SAFARI YA MATUMAINI

13.Naomba Watz wajiandikishe ktk Daftari la Kupiga Kura,watunze Shahada za kupigia Kura ili tuiondoe CCM Madarakani

14.Mimi nauchukia UMASKINI, Kiongozi kujionesha maskini ni upuuzi. Natamani Watz wawe Matajiri km MENGI na AZAM

15.Kulipa kisasi ni upuuzi, umefanya nini mpaka useme nitalipa kisasi? Waulizeni wamefanya nini nilipe kisasi?

16.Kulipa kisasi ni upuuzi, umefanya nini mpaka useme nitalipa kisasi? Waulizeni wamefanya nini nilipe kisasi?

17.Msiwatishe, kama wamefanya madhambi yao waambieni nimewasamehe mimi sitalipa kisasi

18.LIPUMBA- 'UKAWA tumekubaliana maliasili na Rasilimali zitumike kwa manufaa ya Watz wote'

19.MBOWE- 'CCM imekuwa na Wabunge wengi ndani ya Bunge, imefanya waangalie maslahi yao zaidi kuliko Taifa

20.MBOWE- 'Tumekubaliana Wabunge wa UKAWA wakiingia Bungeni November 2015 waangalie zaidi maslahi wa Watz'

21.MBATIA- 'Tunawakikishia Watz kwamba nguvu kubwa ya Serikali ya UKAWA itaangalia maslahi ya Watz'

22.Nilisema mtu ambaye ana ushahidi wowote kuhusu mimi kuhusika na RICHMOND peleka Mahakamani, kama huna kaa kimya

23.Tulikuwa na tatizo la Umeme, tukahangaika kuleta Mitambo ya kuzalisha umeme.

24.Tulipata taarifa kuwa mtu ambaye tunampa kazi ya kuzalisha umeme hakuwa na uwezo

25.Niliondoka Madarakani lakini tatizo limeongezeka, mikono yangu ni misafi mwenye Ushahidi peleka Mahakamani

26.MAKAIDI- 'Nashukuru mmetuletea kifaa LOWASSA, nilimfahamu LOWASSA kupitia mtoto wangu

27.MAKAIDI- 'LOWASSA amekuja UKAWA afuate na Sisi tunavyotaka asahau kidogo mambo ya CCM'

28.MAKAIDI- 'Watanzania wamekwama, najua LOWASSA amekuja UKAWA kutukwamua.. Karibu sana LOWASSA'

29.Salum MWALIMU- 'Kuna taarifa kuwa sehemu kubwa ya Mikoa ya Mbeya, Singida na Arusha umeme umekatwa'

30.MBATIA-'Siku ya leo nina amani kutoka sakafu ya moyo wangu, ninawahakikishia Watz kuwa TZ bila CCM inawezekana'

31.MBATIA- 'UKAWA hatutamwaga damu lakini walio Madarakani wasituchokoze, uwezo wa kupambana kwa hoja tunao'

32.MBOWE- 'Tunapenda kumkaribisha LOWASSA pamoja na familia, marafiki zako na kundi la Watz wapenda haki'

33.MBOWE- 'Ujio wako CHADEMA umezua hofu nyingi kwa sababu hii ni nchi ya hofu'

34.MBOWE- 'Watu wengi wa CCM wamenipigia simu wakasema kumkaribisha LOWASSA ni kuharibu Chama'

35.MBOWE- 'Niliwajibu ni kweli ataharibu Chama, lakini nikajiuliza lini CCM ikawatakia mema CHADEMA?'

36.MBOWE- 'Kumleta LOWASSA kwenye meza hii haikuwa kitu chepesi, tumekaa Vikao viingi usiku na mchana'

37.MBOWE- 'Naongea kwa ujasiri,hatuwezi kufikiri mambo mema mapya kama tutaendelea kufikiri mambo mabaya ya zamani'

38.MBOWE- 'Chama cha Siasa ni watu, mimi niletewe watu Milioni niwakatae mimi ni mwendawazimu?'

39.MBOWE- 'Mimi na Viongozi wa UKAWA hatufikirii kulipiza kisasi'

40.MBOWE- 'Tumeshuhudia Vita ya makundi ndani ya CCM na wengine wakaadhibiwa. Wengi wanalalamika, wanaona ukweli lakini hawana uhuru kuongea'

41.MBOWE- 'Tumeshuhudia Vita ya makundi ndani ya CCM na wengine wakaadhibiwa. Wengi wanalalamika, wanaona ukweli lakini hawana uhuru kuongea'

42.MBOWE- 'Hatujamkaribisha LOWASSA pekeyake, tumemkaribisha na Mamilioni ya Watanzania

43.MBOWE- 'Chama cha Siasa ni watu, mimi niletewe watu Milioni niwakatae mimi ni mwendawazimu?'

44. MBOWE- 'Mimi na Viongozi wa UKAWA hatufikirii kulipiza kisasi'

45.MBOWE- 'Umesaidia kumfungua kifungoni Mbunge Ole MEDEYE na Wabunge wengi ambao tutaendelea kuwakaribisha'

46.MBOWE- 'CHADEMA haiongozwi kwa kauli za MBOWE, inaongozwa kwa Katiba na Kanuni za Chama

47. MBOWE- 'Namshukuru sana Rais JK, umesaidia kutujenga Upinzani kuelekea Uchaguzi wa mwaka huu'

48.MBOWE- 'LOWASSA ujitahidi sana Mazoezi kwa sababu huku kuna mabomu'

49.MBOWE- 'LOWASSA alipokuwa analalamika Dodoma sisi tulikuwa tunafurahi'

50. MBOWE- 'Umesaidia kumfungua kifungoni Mbunge Ole MEDEYE na Wabunge wengi ambao tutaendelea kuwakaribisha
Apple News is seriously good and might become your only news app

Apple News is seriously good and might become your only news app

Apple News is a stripped-back, better alternative to heavy, slow news sites for your phone. You don’t need everyone’s individual apps anymore, just the one, that offers consistent, easy to read and distraction free news.

applenews
Apple News tabsThe app is broken up into a number of tabs. ‘For you’ is a selection of stories from the publications you subscribe to, ‘Favorites’ shows what you’re subscribed to, ‘Explore’ offers suggestions on what to follow and ‘Saved’ is a simple way to save stories for later reading.
Each site can customize their section of the app, but only in very limited ways so that the experience is consistent. Right now, they can change their logo, the background color of the top bar and define the sections news is broken up into.
Stories in the app are presented in a consistent, clean way, though publishers can modify their font and add other elements.
That should be terrifying if your business is making money from online publishing.
The app cuts out the cruft, ad trackers and other elements found on many news sites that can slow loading times.
Readers can swipe up to see an article on its original site, or stick to Apple’s format. With this model there’s few reasons to visit news sites anymore, which is exactly what Facebook’s trying to sell too.
It’s a bold move on Apple’s part to steal more eyeballs from the traditional advertising businesses run by Google and AOL. Apple might as well be yelling that news sites are broken and it’s going to fix them for everyone, whether they like it or not.


While everyone’s panicking about Facebook Instant Articles, I’ve seen something much more terrifying and exciting: Apple News.
The app, which will be installed on every iPhone that upgrades to iOS 9, is a new centralized home for content.
Publishers can input their content via RSS feeds or, if they’re willing to go all-in, add special HTML markup that allows their content to be presented in interesting ways with custom branding in Apple’s app.
Apple News is fast, responsive and enjoyable to use. It puts everything I want to read in a single place, without the need to download a third-party app and it loads incredibly fast, thanks to the company’s content delivery network.
It also recommends new sites you might enjoy following by learning what you read over time.

Kategori

Kategori